Tuesday, September 18, 2012

KUTOKA WIZARA YA ELIMU: WARAKA WA ELIMU NA.5 WA MWAKA 2012 KUHUSU MAREKEBISHO YA MIHULA YA SHULE ZA SEKONDARI NA VYUO VYA UALIMU


Tangu mwaka 2005 kumekuwepo na tatizo la kutofautiana kwa Mihula ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne, Kidato cha Tano na Sita na Vyuo vya Ualimu. Aidha, kipindi cha kufanya mitihani ya Taifa katika kidato cha Nne na Sita hutofautina. Vilevile, usahihishaji wa mitihani ya ngazi hizo za elimu umekuwa ukifanyika wakati baadhi ya makundi ya wanafunzi wakiendelea na masomo Shuleni/Vyuoni.

Usahihishaji wa mitihani wakati baadhi ya makundi ya wanafunzi wakiendelea na masomo umekuwa ukiathiri maendeleo ya wanafunzi kimasomo. Wasahihishaji wa mitihani hiyo wamekuwa na muda mrefu wa kufanya kazi hiyo na kukosa muda wa kupumzika na kujikuta wanafanya kazi hiyo kwa mfululizo mwaka mzima. Hali hiyo imesababisha baadhi ya walimu kushindwa kufanya kazi za kitaaluma ipasavyo.

Ili kurekebisha hali hiyo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeamua kurekebisha Mihula ya shule; ili wanafunzi wa ngazi zote katika shule za Msingi, Sekondari na Vyuo vya Ualimu wawe na vipindi vya likizo vinavyofanana.

Aidha, urekebishaji wa Mihula utaendana sambamba na marekebisho ya vipindi vya mitihani ya Taifa katika ngazi hizo kama ifuatavyo:
Tanbihi: Wanafunzi wote watapumzika Mwezi Juni na Desemba. Waraka huu, unaanza kutumika tarehe 01 Januari, 2013 na kufuta Waraka wa Elimu Na. 5 wa Mwaka 2004
 
M. M. Wassena
KAIMU KAMISHNA WA ELIMU
Nakala:
Katibu Mkuu,
OWM -TAMISEMI,
S.L.P. 1923,
DODOMA.
Mkurugenzi,
Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima,
S.L.P. 20679,
DAR ES SALAAM.
Mkurugenzi Mkuu,
Taasisi ya Elimu Tanzania
S.L.P. 35094,
DAR ES SALAAM.
Katibu Mtendaji,
Baraza la Mitihani la Tanzania,
S.L.P. 2624,
DAR ES SALAAM.

No comments:

Post a Comment